Kilimo cha Mtama

Share:
Mtama ni zao la chakula na biashara. Ni zao muhimu katika maeneo yanayokabiliwa na ukame. Na pia sehemu ambazo udongo una rutuba ya wastani. Utafiti wa zao hili umeweza kutoa teknolojia mbalimbali ambazo zinaweza kutumiwa ili kuongza tija katika uzalishaji. Teknolojia hizi ziko kwenye uwezo wa wakulima.
Utayarishaji wa shamba
Tayarisha shamba ili udongo uwe laini kurahisisha uotaji. Kama shamaba limelimwa na trekta inabidi lipigwe haro na ikiwa imetayarishwa kwa jembe la mkono. Mabonge mabonge ya udongo yanatakiwa yavunjwe.

Kiasi cha mbegu
Upandaji kwenye mistari pasipo kupunguzia kunahitaji kilo 7 hadi 8 kwa hekta na upandaji kwa mashine unahitaji kilo 8 hadi 10 kwa hekta
Upandaji
Unaweza kupanda kwenye vumbi kabla ya mvua kunyesha au wakati wa mvua zinapoanza au wakati mvua zimenyesha za kutosha kina: kupanda kwenye vumbi cm 5.0-6.0; kupanda kwenye udongo wenye unyevu 2.5-4.0 nafasi. Sehemu za unyevu mwingi: 60cm-20cm (cm 60 kati ya mstari an mstari na cm 20 kati ya shina na shina); Maeneo ya makame: cm75 x cm 20 au cm 90 x cm 30

Mbolea
Aina mbalimbali za mbolea na samadi zinatumika kuongeza ratiba ya udongo.
Samadi; Inatakiwa isambazwe kwenye shamaba na kulimiwa chini au iwekwe kwenye mistari na kuchangwa na udongo kabla ya kupanda. Kiasi kilichopendekezwa ni kiasi cha 5-10 kwa hekta na iwekwe mwezi mmoja kabla ya kupanda.

Mbolea
Kabla ya kupanda; mbolea aina ya DAP, 20:20:0, 23:23:0 katika kiwango cha kg 20 N na – 20 kilo P205 kwa eka, iwekwe wakati wa kupanda na kabla ya kupanda mbegu .
Top dressing: kilo 20 N za mbolea aina ya urea, CAN iwekwe pembeni ya mimea na hakikisha kuna unyevu wa kutosha wa kuyeyusha mbolea vizuri .

Palizi
Palizi lifanyike mara mbili. Palizi la kwanza lifanyike wiki 2-3 baada ya mbegu kuota. Dawa za kuua wadudu zinazoweza kutumika ni laso au gesaprim (kabla ya kuota) 2,4 D (baada ya kuota)

Kupunguzia
Mimea ipunguziwe ikiwa na wiki 3-4 baada ya kuota na ipunguziwe wakati udongo una unyevu wa kutosha kupunguza madhaa kwa mimea.

Ukame na aina ya udongo
Ukame ni moja wapo ya madhara makubwa yanadhuru mtama unaotegemea mvua. Ukame unaweza kutokea kabla au baada ya kuchanua. Madhara ya ukame yanaweza kuepukwa kwa kupanda mapema na kupanda mapema mapema aina ya mbegu zinazowahi au kuvumilia ukame au kutumia mbinu mbalimbali za kuifadhi maji.
Wadudu waharibifu
 I) Inzi wa bua (Atherigona soccata), Madhara yanatokea siku 7 hadi 30 baada ya kuota. Viluwiluwi wanakula ndani ya mmea na kusababisha dalili za moyo kufa (dead heart). Ucheleweshaji kupanda huongeza madhara.
 ii) Vitoboa -bua (sterm borers Chillo partellus), Dalili ni vidirisha vidogo kwenye majani machanga, viluwiluwi hutoa bua na mimea michanga inayoonyesha mioyo kufa (deadheart)