Mbegu za GMO ni Siasa Chafu

Share:

Katika miaka ya hivi karibuni Watanzania tumekua tukisikia kuhusu swala la kuwekeza katika kilimo ambacho wanasiasa wanakiita "KILIMO CHA KISASA" ambacho kinahusisha utumiaji wa mbegu ambazo ni Genetically Modified. Lakini ni nini hasa maana ya GMO?, Je ni salama kwa kula?.

GMO ni aina ya mbegu na mimea ambayo imebadilishwa vinasaba (genes) katika maabara ili kuboresha aina fulani ya traits au tabia inayohitajika, kwa mfano kuongeza virutubisho, na kuongeza uwezo wa kujikinga na madawa.

Marekani ndio inaongoza kwa utengenezaji wa aina hii ya mbegu zikizambazwa na makampuni kama Monsanto, Syngenta AG, na DOW Chemicals ambazo nyingi tumekua tukiziona nchini. Hatari zitokanazo na aina hii ya mimea ni nyingi kuliko faida, na nchi nyingi duniani tayari zimezuia matumizi ya aina hii ya mbegu ikiwemo Canada, Argentina, Australia, India na Mexico na msimamo wa EU Ukiwa "Zuia GMO".

Msomi mmoja wa Chuo Kikuu Cha elimu ya juu cha Nelson Mandela alisema baadhi ya athari za GMO ni; Kuharibu mfumo wa ikolojia, kuharibu ama kubadilisha kabisa virutubisho katika mimea, Kansa, kuharibu rutuba ya ardhi na kusababisha wakulima kua tegemezi wa madawa ya kilimo, kujitokeza kwa magugu ambayo yanajikinga na madawa ya kuua magugu, na hasara kwa wakulima kutokana na ununuzi wa kiasi kikubwa cha madawa.

Faida chache alizonitajia ni pamoja na ongezeko la mimea inatojikinga na wadudu na magonjwa, kuongezeka kwa food supply, na kua na mimea inayostahimili ukame. Pia aliniambia "Hakuna Mwanasayansi duniani ambaye yuko serious atakayetoa support kwa GMO, UNLESS yuko katika payroll ya hayo makampuni", kwa sababu kiuhalisia, ni makampuni ya Biotech ambao ndio watengenezaji na wasambazaji watakaonufaika kutokana na mauzo ya mbegu na madawa!

Swali la kujiuliza; Je ni Watanzania wangapi wanazijua athari zitokanazo na GMO's?, au wengi wetu tumeangalia faida za kiuchumi kuliko athari za kimaziangira na kiafya?. TUAMKE NDUGU ZANGU!!