Mbaazi
ni zao ambalo ni jamii ya mikunde. Zao hili hustahimili ukame na
huzalishwa kwenye maeneo mengi hapa nchini. Karibu mikoa yote
Tanzania hulima mbaazi kama zao la chakula na biashara. Zao hili
linastawi kwenye mwinuko wa mita 0- 2000 kutoka usawa wa bahari.
MAZINGIRA
BORA
Hali
ya hewa
Mbaazi
hutaawi kwenye maeneo yenye kupata mvua za chini (mm 500) hadi
zinazopata mvua za kutosha (mm 1500)
Aina
ya Udongo
Mbaazi
hustawi vizuri karibu katika aina zote za udongo wenye rutuba ya
kutosha. Udongo usiotuamisha maji unapendekezwa katika uzalishaji wa
zao hili.
SIFA
YA SHAMBA
Historia
ya shamba
Mzalishaji
aepuke kuzalisha mbegu kwenye shamba ambalo msimu uliopita lilipandwa
mbaazi, isipokuwa kama mbaazi zilikuwa za jamii (aina) ile ile na
daraja la juu.
Utenganisho
wa shamba
Shamba
la mbaazi linatakiwa kutengwa kutoka shamba lingine la mbaazi kwa
umbali wa mita 50.
Sifa
za ziada katika uzalishaji wa mbegu
Mzalishaji
anapaswa awe na utaratibu kwa kutopanda mfululizo zao hili katika
shamba moja ili kuepuka magonjwa kama mnyauko wa mimea
UTAYARISHAJI
WA SHAMBA
Shamba
jipya
Shamba
jipya lafaa kung'olewa visiki kabla ya kuanza kutifua ardhi
Shamba
la zamani
Shamba
la zamani linaweza kutifuliwa kwa kutumia aidha wanyama kazi, jembe
la mkono au trekta. Hakikisha kwamba shamba limetifuliwa kina cha
kutosha na mabonge yapigwe ili kupata udongo laini.
Chanzo
cha mbegu
Mbegu
zitakazotumika katika uzalishaji zisiwe chotara. Mkulima atumie mbegu
ya daraja la msingi, au kuthibitishwa ama QDS 1. Mbegu ya msingi na
iliyothibitishwa hupatikana katika mashamba ya wakala wa mbegu za
kilimo (Agricultural Seed Agency-ASA). Vilevile mbegu za daraja la
kuthibitishwa hupatikana katika makampuni ya mbegu, kupitia kwa
wakala wao au maduka ya pembejeo.
Mkulima
anaruhusiwa kutumia mbegu ya QDS 1 iliyopatikana kutoka kwa mkulima
wa mbegu aliyesajiliwa na TOSCI, kama chanzo cha mbegu, lakini ajue
ya kwamba, akishavuna haezi kuitumia kama mbegu tena. Aina ya mbegu
zinazopendekezwa na wizara ya kilimo ni komboa, mali, tumia.
UPANDAJI
WAKATI
WA KUPANDA
Mzalishaji
anashauriwa kuzalisha mbegu wakati wa mvua za msimu. Mbaazi za muda
mfupi hustawi zaidi ukanda wa chini na ni vyema zikapandwa mwishoni
mwa mwezi wa Februai kwani hukomaa katika muda wa siku 120.
Mbaazi
za muda mrefu hustawi vema kwenye ukanda wa kati na wa juu na
huchukua muda wa siku 180 kukomaa. Aina hizi zipandwe mwezi Disemba
na Januari.
Kiasi
cha mbegu
Ili
kupanda ekari moja unahitaji kilo 3 za mbegu ya muda mfupi na kilo 2
za mbegu ya muda mrefu.
NAFASI
YA KUPANDA
Mbaazi
za muda mfupi
Panda
kwa umbali wa sentimita 50 kati ya mistari na sentimeta 20 kati ya
mashina. Panda mbegu 2 kila shimo, mwishoni bakiza shina moja tu.
Mbaazi
za muda mrefu
Panda
kwa umbali wa sentimeta 180 kati ya mstari na sentimeta 50 kati ya
mashina. Panda mbegu 2 na mwishoni bakiza mmea 1 kwa kila shina.
MATUMIZI
YA MBOLEA
Mbaazi
ikiwa ni zao jamii la mikunde hutengeneza mbolea ardhini, hata hivyo
ni vyema mzalishaji arutubishe shamba lake ili kupata mavuno mengi.
Tumia samadi iliyoboreshwa kama mbolea ya kupandia. Usitumie mbolea
za kukuzia kwani mbaazi huwa zinajitengenezea zenyewe virutubisho
vya kujikuzia.
KUSAJILI
SHAMBA LA MBEGU
Mara
baada ya kupanda, mzalishaji analazimika kusajili shamba lake katika
Taaasisi ya udhibiti wa ubora wa mbegu (TOSCI) aidha katika kituo cha
Mororgoro, Njombe au Arusha au sehemu nyingine ambazo taasisi hiyo
ina ofisi katika muda usiozidi siku 30 ili kutoa nafasi wakaguzi hao
kupanga utaratibu wa ukaguzi.
PALIZI
Hakikisha
shamba linakuwa safi kwa kupalilia mara kwa mara katika wiki 6 za
mwanzo. Baada ya hapo palilia tu inapobidi kufanya hivyo.
KUNG'OA
MIMEA ISIYOFAA NA YENYE UGONJWA
Toa
mimea yote ambayo haifanani na mimea husika, pia ondoa mimea yote
yenye ugonjwa
UDHIBITI
WA MAGONJWA NA WADUDU WAHAIBIFU
Magonjwa
Mbaazi
hushambuliwa na magonjwa ya mnyauko, mzalishaji aonapo mmea wenye
dalili hizi aung'oe na kutupa nje ya shamba.
Uzuiaji
Wadudu
Mbaazi
za muda mfupi, hushambuliwa sana na wadudu, Nyunyiza dawa za asili za
kuua kudhibiti wadudu waharibifu mara tu zinapoanza kutoa maua hadi
kukomaa. Muulize afisa ugani wako namna ya kutengeneza madawa ya
asili yanayokubalika katika mfumo wa kilimo hai.
UKAGUZI
WA SHAMBA LA MBEGU
Ili
kuhakikisha kuwa taratibu zote zinazotakiwa kufuatwa kwa ajili ya
kuzalisha mbegu za kilimo hai zimezingatiwa, shamba la mbegu lazima
likaguliwe. Ukaguzi wa nje unafanywa na shirika la Kilimo hai
Tanzania na wataalamu kutoka taasisi ya kudhibiti uboa wa mbegu
(TPSCI). Wataalamu wa TOSCI wanakagua shamba la mbegu mara tatu kabla
y kuchanua, wakati wa kuchanua na kabla ya kuvuna.
UVUNAJI
WA MBEGU
Dalili
za kukomaa
Wakati
wa kukomaa na kukauka vitumba hubadilika rangi na kuwa kahawia.
Namna
ya Kuvuna
Vuna
kila baada ya siku 3 hadi 5 kwa kuchuma vitumba au kukata matawi.
Kukausha
Mbegu
Mavuno
yote ambayo yametolewa shambani yapelekwe moja kwa moja kwenye
kiwanja cha kukaushia. Ni vizuri sana kukaushia mbegu zilizo vunwa
kwenye mkeka au sakafu safi isiyo na unyevunyevu.
Kupura
Mbegu
Weka
vitumba kwenye gunia halafu upige kwa kutumia fimbo ndogo, ili
kuibanguwa.
KUSAFISHA
MBEGU
Kutoa
uchafu
Peta
mbegu kwa kutumia ungo na upepo. Ondoa uchafu wote na mbegu safi
ziwekwe kwenye chombo kisafi. Chambua mbegu zilizo kuwa na rangi
tofauti na zenye magonjwa zitupwe au zitunzwe kwa ajili ya chakula.
Vile vile mbegu zilizonyong'onyea zitengwe.
Kuhifadhi
Mbegu
Hifadhi
mbegu katika mifuko misafi, mahali penye mzunguko mzuri wa hewa na
pasipo wadudu waharibifu. Vichanja huweza kutumika kuzuia mbegu
kupata unyevunyevu wa sakafu. Changanya mbegu na majivu ya jikoni au
dawa nyingine za asili kudhibiti wadudu. Tunza mbegu mbali na madawa
hatari na chakula.