Mahindi
ni zao linalolimwa karibu kanda zote za Tanzania. Zao hili hustawi
vizurio zaidi katika maeneo yaliyo kati ya mita 0 – 2400 kutoka
usawa wa bahari na hii inawezesha kuwa na aina nyingi za mahindi za
muda mfupi, kati na mrefu
Mahindi
ni chakula kikuu cha watanzania na huzalishwa sehemu nyingi hapa
nchini, hivyo uzalishaji wa mbegu za mahindi ni muhimu katika
kuboresha uzalishaji na tija katika kupata mavuno yaliyo bora.
Kila
mzalishaji wa mbegu awe amepata mafunzo ya awali na kusajiliwa.
MAZINGIRA
BORA
Hali
ya hewa
.
Mahindi hustawi vizuri eneo lenye wastani wa mvua wa mm 700 – 1800
kwa mwaka zenye mtawanyiko mzuri.
.
Mahindi huota vizuri kwenye udongo unaopitisha maji
.
Mahindi hustawi vizuri kwenye shamba lenye rutuba na linalotuamisha
maji.
SIFA
ZA SHAMBA
Historia
ya shambani
Shamba
ambalo halikulimwa mahindi msimu uliopita linafaa kwa uzalishaji
mbegu za mahindi iwapo unataka kulima mahindi katika eneo lilelile
unaweza kutukia mbegu za aina ile ile.
Utengaji
wa shamba la mbegu
Tenga
shamba lako kutoka kwenye aina na daraja lingine la mahindi mita 190
pande zote kutoka kwenye shamba lingine la mahindi. Tenganisha kwa
muda wa siku thelathini (30) ukizingatia aina ya mbegu ya mahindi.
Sifa
za ziada
Zingatia
ubadilishaji wa mazao katika shamba lako; usipande zao lamahindi kwa
muda wa misimu miwili ya uzalishaji. Kabla hujarudishia mahindi
katika shamba lako panda mzao ya mikunde. Shamba lako lamahindi
lisiwe na historia ya gugu aina ya kiduha (striga).
Utayarishaji
wa shamba
Ukiisha
chagua eneo lako lima kwa kina, endapo majani au magugu ni mengi
shambani, inakubidi ulime angalau mwezi mmoja kabla yaq kupanda ili
majani yaoze vizuri. Iwapo shamba lako ni la zamani lima kwa kina na
lainisha udongo ili kiruhusu maji kupenya ardhini.
Chanzo
cha mbegu
Mbegu
zinakazotumika katika uzalishaji ziwe chotara. Mkulima atumie mbegu
ya daraja la msingi, au kuthibitishwa ama QDS 1. Mbegu ya msingi na
iliyothibitishwa hupatikana katika mashamba ya wakala wa mbegu za
kilimo (Agricultural Seed Agency). Vilevile mbegu za daraja la
kuthibitishwa hupatikana katika makampuni ya mbegu, kupitia kwa
wakala wao au maduka ya pembejeo.
Mkulima
anaruhusiwa kututumia mbegu ya QDS 1 iliyopatikana kutoka kwa mkulima
wa mbegu aliyesajiliwa na TOSCI, kama chanzo cha mbegu, lakini ajue
ya kwamba, akishavuna hawezi kutumia kama mbegu tena.
Aina
ya mbegu zinazopendekezwa na wizara ya kilimo ni staha, kilima, kito,
katumani, TMV.1, TMV.2, Tuxpeno
Angalizo
Kwa
mkulima anaenza kuzalisha mbegu, anashauiwa kutumia mbegu ya daraja
la msingi.
UPANDAJI
Wakati wa kupanda
Kwa
matokeo mazuri ya mavuno ya mbegu panda wakati wa mvua za mwaka
(masika). Vile vile mkulima atambue muda wa kukomaa, na avune wakati
mvua zinakwisha.
Kiasi
cha mbegu
Tumia
kilo 8 – 10 kwa ekari na kilo 20 – 25 kwa hekta.
Nafasi
ya kupanda
Mahindi
yanaweza kupandwa kwa kutumia nafasi zifuatazo
i)
sm 75 x 30 (tumia mbegu mbili) katika shimo na ng'oa bakiza mche
mmoja baada ya kuota.
ii)
sm 75 x 60 (mbegu tatu) kwa shimo, ng'oa moja bakiza mbili.
Matumizi
ya mbolea
.
Rutubisha udongo kwa kutumia samadi iliyoboreshwa au mboji
.
Mbolea za kukuzia ni: chai ya samadi na chai ya mmea
Kusajili
shamba la mbegu
Mara
baada ya kupanda, mzalishaji analazimika kusajili shamba lake katika
Taasisi ya udhibiti wa ubora wa mbegu (TOSCI) aidha katika kituo cha
morogoro, Njombe au Arusha au sehemu au sehemu nyingine ambazo
taasisi hiyo ina ofisi katika muda usiozidi siku 30 ili kutoa nafasi
wakaguzi hao kupanga utaratibu wa ukaguzi.
Palizi
Palilia
shamba lako la mbegu ya mahindi mapema na hakikisha shamba lako
linabaki safi wakati wote
Magugu
hatari
Magugu
hupunguza mavuno, hivyo ni muhimu kupalilia mapema, pia shamba lako
la mbegu lisiwe na historia ya gugu aina ya kiduha (striga)
Kung'oa
mimea isiyofaa na yenye ugonjwa
Ondoa
mimea yenye magonjwa na iliyoharibiwa na wadudu, pia ondoa
machipukizi,
Zingatia
Shughuli
hii lazima ifanywe kwa kushirikiana na afisa ugani aliye karibu nawe.
Udhibiti
wa Magonjwa na Wadudu waharibifu
.
Hakikisha kwamba mimea yote yenye virusi na milia (maize streak virus
inaondolewa)
.
hakikisha unaondoa na kufukia mazao yaliyo na fugwe (smut disease).
Udhibiti
wa magonjwa na wadudu waharibifu
.
Hakikisha kwamba mimea yote yenye virusi wa milia (maize streak
virus inaondolewa.
.
Hakikisha unaondoa na kufukia mazao yaliyo na fugwe (smut disease)
Wadudu
Waharibifu
.
Fanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kuangalia viwavi jeshi na
kuwadhibiti kwa kutumia madawa yanayoshauriwa na wataalam wa ugani
ambayo yanakubalika katika mbinu za kilimo hai.
.Tumia
dawa za kuzuia Sondo, kwa kutumia viatilifu vya asili.
I
Wanyama
Waharibifu
.
Zuia wanyama waharibifu kwa kulinda, motego na kuwaarifu maafisa
wanyama pori.
Ukaguzi
wa Shamba la Mbegu
Ili
kuhakikisha kuwa taratibu zote zinazotakiwa kufuatwa kwa ajili ya
kuzalisha mbegu za kilimo hai zimezingatiwa, shamba la mbegu lazima
likaguliwe, Ukaguzi wa ndani unafanywa na wataalamu husika kutoka
miongoni mwa wanakikundi. Ukaguzi wa nje unafanywa na shirika la
kilimo hai Tanzania na wataalamu kutoka taasisi ya kudhibiti ubora wa
mbegu (TOSCI). Wataalamu wa TOSCI wanakagua shamba la mbegu mara tatu
kabla ya kuchanua, wakati wa kuchanua na kabla ya kuvuna.
Uvunaji
wa mbegu
.
Mazao yavunwe mara baada ya ukaguzi wa mwisho.
.
Vuna mahindi yaliyokomaa na kukauka vizuri mbegu zinazovunwa mapema
mno hazizalishi mimea yenye afya. Dalili za mbegu ya mahindi kukomaa,
kuonekana na doa jeusi kwenye gunzi.
Namna
ya Kuvuna
Kuna
namna mbili kuu za kuvun:
.
kwenye mahindi; menya na kuweka kwenye mfuko
.
Kata bua kutoka chini, halafu simamisha shambani kuelekea upepo
utakapo
Ukaushaji
Kausha
mbegu zako katika kichanja chenye paa kuzuia jua. Kausha mbegu kwa
kupanga mabua kwa kusimamisha na yapange mithali na nyumba ya
mmgongo punda
Uchambuzi
wa mbegu
Chambua
mahindi katika sehemu safi, ondoa yenye matatizo kama magonjwa,
yasiyo komaa na yaliyopoteza sifa za mahindi na weka mbali mahindi
yasiyo na sifa.
Kupukuchua
Pukuchua
mbegu ya mahindi kutokana na nzi uliyoyachagua kama mbegu, usichukie
mahindi yaliyoanguka au usichanganye mahindi yaliyoanguka ili
kuhakikisha mbegu imekauka vizuri; jaribu kwa kung'ata kwa meno iwapo
utasikia mlio tambua mbegu haijakauka vizuri.
Kuna
aina tatu za kupukuchua:
.
Kwa kutumia mkono
.
Kwa kutumia mashine.
.
Kwa kupiga kwenye gunia
Njia
nzuri ni ya kutumia mkono ijapo kuwa huchukuwa muda mrefu, lakini ni
salama zaidi kwani mbegu hazivunjiki.
Kupeta
Peta
kwa kutumia ungo; ama kwa kutumia upepo.
Kuhifadhi
mbegu
.
Sehemu ya kuhifadhi iwe safi.
.
Kihenge au ngoko kiwe kinazuia panya kuharibu mbegu.
.
Chumba cha kutunzia mbegu kiwe kinapitisha hewa kwa urahisi. Pata
ushauri wa wataalamu wa kilimo hai katika matumizi ya mbinu/ madawa
ya asili kwa ajili ya kuhifadhi mbegu.
Vifaa
vya kuhidhia mbegu
.
Tumia vifaa safi, kama vile magunia, na mifuko au madebe.
.Panhga
magunia yasigusane na ukuta na sakafu ili kuruhusu mzunguko wa hewa
na ukaguzi.
.
Weka utambulisho katika kila kifaa kilichowekwa mbegu.