UTUNZAJI ASILIA ZINAZOFAA KWA UTUNZAJI ASILIA WA MAZAO

Share:

Ili kutekeleza utunzaji asilia wa mazao ni muhimu sana kuelewa mbinu asilia za kufanikisha kilimo. Kwa hali hiyo matukio ya majanga ya kushambuliwa na wadudu wahaibifu yanaweza kupunguzwa na utumiaji wa hatua za utunzaji wa mazao.

I) KUELEWA MFUMO WA UHUSIANO WA VIUMBE NA MAZINGIRA YA KILIMO
. Aina za wadudu waharibifu na wadudu waharibifu na wadudu wenye manufaa katika shamba illolimwa na katika neo la jirani.

. Biologia ya wadudu waharibifu. Magonjwa naa wadudu wenye manufaa (maumbile. Mzunguko wa maish, tabia ya kuuzana, taabia za kula n.k).

. Utaratibu unaojirudia wa wadudu katika msimu mbalimbali na kutegemea kwao hali ya mazingira.

. Aina ya madhara wakati wa mzunguko wa maisha ya wadudu yatakayosaidia katika mbinu zaidi za kuwadhibiti vizuri.

. Msimu au hatua ya ukuaji wa mmea shabani ambapo ni hatari zaidi kushambuliwa na wadudu.

. Mimea mingine (inayolimwa au ya porini) inayowavutia wadudu maalumu waharibifu.

. Wadudu marafiki au vimelea wanaoweza kutumiwa kuwala wadudu hao waharifu.

. Wadudu marafiki au vimelea wanaoweza kutumiwa kuwala wadudu hao waharibifu.

ii) KILIMO MCHANGANYIKO CHA AINA MBALIMBALI
Mazao ya aina mbalimbali yanayolimwa sambamba na maua au mimea ya porini yatasababisha mfumo wa aina tofauti utakaosaidia kuwepo kwa maskani na chakula kwa aina mbalimbali za ndege, wadudu na wanyama watambao (jamii ya mijusi); ambapo pia hupunguza aina fulani fulani ya wadudu waharibifu wa mazao.

iii) HALI YA ARDHI
Maeneo yanayolimwa kama vile miteremko mikali ya milima, maeneo yasiyofikia au yaliyozungushwa mimea ni maskini mazuri kwa ndege, wadudu na wantyama watambaao (jamii ya mijusi) wanaowinda wadudu waharibifu.

iv) KUBADILISHA MAZAO NA KUCHANGANYA MAZAO
Madhumuni makubwa ya kubadili maazao ni kutenganisha aina fulani ya wadudu waharibifu, wa zao fulani; ambao kukosekana kwa zao hilo huwafanya wahame au kufa kwa kipindi hicho. Hivyo ni vizuri kubadilisha mazao ambayo si ya jamii moja; katika msimu unaofuata, yaani mazao yanayo shambuliwa zaidi na mdudu fulani, sharti yabadilishwe na yale ambayo mdudu huyo hayapendelei. Kwa mfano: ili kuzuia bungua wa mahindi; ni vizuri baada ya kuvuna mahindi msimu unaofuata maharagwe yaoteshwe. Hali hii huharibu mzunguko wa maisha ya bungua wa.
Ni vizuri pia kuchanganya mazao ili kupunguza mashambulizi ya wadudu.

V.MATUKIO ASILIA YANAYOJIRUDIA NA WAKATI MUAFAKA WA KUPANDA
Kuchagua wakati muafaka wa kupanda kunaweza kupunguza mashambulizi. Kufahamu mzunguko wa maisha ya wadudu na mahusiano yake katika mazao yanayo shambuliwa humrahisishia mkulima kuchagua muda wa kupanda. Kutokana na hili mkulima anaweza kupanda mapema au kuchelewa kupanda, ili kuepuka kipindi ambacho wadudu huzaliana kwa wingi.

Kwa mfano: nyanya zilizopandwa wakati wa kiangazi hazipati magonjwa ya ukungu kwani hakuna maji yakuzidi kiasi yanayolowanisha majani ili kuwezesha vimelea vya ukungu kuota.


VI. KUTIA MBOLEA NA AFYA YA MIMEA
Mimea yenye afya nzuri zaidi hustahimili athari iletwayo na magonjwa na wadudu waharibifu na kutoa mavuno mengi. Mbolea huwa na wadudu marafiki ambao hurutubisha ardhi.

VII. ULIMAJI ARDHI
Utifuaji wa ardhi kwa jembe la kukokotwa na ng'ombe au trekta un alengo la kuuairisha funza na hatua nyingine ya kukua kwa wadudu waharibifu waliobaki ardhini au kwenye mabua ya mazao. Kwa kuwachimbua wataunguzwa na jua na kulikuwa na wanyama au ndege. Mabaki ya mazao hufukiwa na hivyo kukutana na viumbe wa ardhini na unyevunyevu ambao huyaozesha na kurutubisha ardhi.

VIII. UTEUZI WA AINA BORA YA MBEGU
Uteuzi wa aina ya mbegu inayostahamili wadudu au magonjwa husababisha wadudu waharibifu na magonjwa kushindwa kuzaliana.

IX. USAFI WA SHAMBA
Usafi wa shamba husaidia kuharibu mzunguko wa maisha ya wadudu waharibifu, wadudu waharibifu hukosa masikani.

X. KUPANDA KWA NAFASI
Kupunguza kivuli, kupunguza matawi, kuondoa maotea na kushikilia mimea kwa miti ili isilale ardhini: Matendo yote haya husababisha mazingira yasiwe mazuri kwa maendeleo ya vimelea vya magonjwa na wale wadudu waharibifu wapendao kuishi kwenye hali ya kivuli.

XI. MASUALA YA KIJAMII
Utunzaji wa mimea ni jukumu la jamii nzima. Mkulima binafsi hawezi kamwe kuchukua hatua zinazofaa kupambana na wadudu waharibifu wanaoenea sehemu kubwa mwenyewe.


Hapa ni mahali pazuri pa kufikiria kushirikiana na majirani ili kuchukua hatua ya pamoja kukabiliana na janga la wadudu.