KUPANDA NDIZI KWA MBINU ZA KILIMO HAI

Share:

UTARATIBU WA USIMAMIZI WA BUSTANI YA NDIZI
Usimamizi sahihi huimarisha mimea na hupunguza kuenea kwa wadudu na magonjwa.

- Weka mazalia 3 hadi 4 kwa shina

- Ondoa majani ya zamani kwani yanaficha magonjwa

- Acha majani 8 hadi 10 wakati mgomba unabeba, na 4 wakati wa kuvuna

-Tumia majani yaliyoondolewa kama matandazo.

- Ondoa machipukizi dume ili ku-punguza kuenea kwa ugonjwa

UDHIBITI WA MAGONJWA NA WADUDU

Kilimo hai kinasisitiza kuzuia maambukizi na kuenea kwa wadudu na magonjwa.

- Tumia aina zinazohimili magonjwa

- Tumia vifaa safi kwa ajili ya kupanda

- Hakikisha usafi wa shamba

- Eneo kuzunguka shina lisiwe na kitu chochote.

- Ongeza rutuba ya udongo.

- Haribu mashamba yaliyojaa ugonjwa na usipande ndizi kwa mwaka 1 hadi 2.

KUBORESHA RUTUBA YA UDONGO
Hifadhi ya udongo na maji

- Jenga uzio na panda mazao ya kufunika ardhi kuzuia maji kupotea na mmomonyoko wa udongo.

- Tumia miti ya kivuli na matandazo kuhifadhi unyevu wa udongo

Mbolea za kilimo hai
- Tumia mboji katika kupanda miche mashimo

- Ongeza mbolea kwa juu kabla tu ya kuchanua

KILIMO MSETO CHA NDIZI NA UDHIBITI WA MAGUGU
Mfumo wa ghorofa
Ghorofa ya juu
- Tumia miti ya kivuli kukinga dhidi ya upepo na kudhalisha mbao

Ghorofa ya kati
- Panda miti ya matunda, kakao na kahawa kushamirisha uzalishaji wa ndizi

Ghorofa ya chini
- Panda mazao ya kila mwaka na
mazao ya mikunde yanayofunika
udongo.

- Kupalilia kwa muda stahiki huon-
doa ushindani wa magugu na
magonjwa.

UTUNZAJI SAHIHI BAADA YA KUVUNA NA UPATIKANAJI WA SOKO
- Hifadhi sahihi baada ya kuvuna huzuia ubora kupungua.

- Mazao bora ya kilimo hai yana soko kubwa nje ya nchi.

-  Shirikianeni na wakulima wengine kupunguza gharama za uthibitisho