FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA NYANYA

Share:
Nyanya
ni mmea wa familia Solanaceae, ambao daima hutambaa na ambao hukuzwa kwa makusudi ya kutumiwa na watu. Matunda yake yanaitwa nyanya. Kwa aina nyingi sana nyanya huwa na rangi nyekundu pindi inapoiva, nyingine zina rangi ya manjano au machungwa. Mnyanya huwa na urefu wa mita 1-3 na huwa na shina laini ambalo mara nyingi hujibebelesha kwenye mmea mwingine. Majani huwa na urefu wa sentimeta 1-25, na petali 5-9 Majani ya shina la nyanya huwa na vinyweleo. Maua huwa na upana was m 1-2, rangi ya manjano na majani matano na huvunwa kwa mwaka mmoja. na K, potasiamu na nyuzinyuzi

Nyanya zina aina mbalimbali za viasili vya kurutubisha na visivyorutubisha vinavyohusiana na faida kadha wa kadha za kiafya. Hii inajumuisha lycopene, vitamini C, A na K, na K, potasiamu na nyuzinyuzi

Faida za nyanya kiafya za nyanya katika mwili ni kama zifuatazo
-Kuusaidia mwili kudumisha viwango vya lehemu vyenye kuleta afya bora.

-Kuongeza uzalishaji wa nishati

-Kuweka katika hali ya kawaida kikemikali cha kusawazisha sukari ya damu (insulin) na kuzuia ongezeko la uzito wa mwili linaloweza kuhatarisha afya.

-Kuulinda mwili dhidi ya uharibifu utokanao na chembechembe za maradhi na kuukinga na uzee wa kabla ya wakati

-Kudumisha mfumo wa kinga ya mwili, mfumo wa umeng’enyaji, kudumisha afya ya viungo vya mwili na mifupa

-Kuweka msukumo wa damu katika kiwango bora cha afya.