Kuna madhara mengi yatokanayo na matumizi ya
dawa za viwandani zenye sumu. Madhara hayo ni
pamoja na athari za afya kwa binadamu, wanyama,
mimea, na uharibifu wa mazingira pamoja na vyanzo
vya maji.
Dawa za asili zinazoweza kusaidia kudhibiti magonjwa ya mazao
Vitunguu saumu
Dawa hii hutumika kufukuza wadudu kutokana na harufu yake. Chukua gramu 100 za vitunguu, twanga
vilainike, changanya na maji lita mbili. Chuja kisha nyunyiza kwenye mimea. Dawa hii pia inaweza
kuchanganywa na mojawapo ya dawa za asili, ili kutoa harufu kali itakayofukuza wadudu.
Majivu
Weka majivu moja kwa moja kwenye mashina ya mimea michanga baada ya kuotesha ili kuzuia wadudu
wakatao mimea michanga. Majivu huonyesha matokeo mazuri endapo yatachanganywa na mafuta ya taa
kidogo.
Ndulele/ ndula
Chukua matunda ya ndulele 30 au 40 haijalishi yameiva au mabichi. Katakata na uyakamue ili kupata
juisi. Ongeza lita moja ya maji, koroga sawa sawa kisha chuja. Ongeza maji lita mbili. Tumia lita moja ya
dawa kwa lita 15 za
Maji kisha nyunyiza mimea mara mbili kwa wiki.
Pilipili kali
Hii ni moja ya dawa za asili ambazo zimekuwa zikitumika na kwa ufanisi mkubwa. Dawa hii
inapotengenezwa na kutumika kwa umakini huwa na ufanisi mkubwa zaidi katika udhibiti wa wadudu na magonjwa.
Chukua gramu 55 za pilipili. katakata vipande vidogo vidogo kisha chemsha kwa dakika 20 kwenye
maji ya lita tano. Chuja kisha ongeza maji lita 5 Dawa hii huua wadudu wenye ngozi ngumu (mbawa
kavu) na laini kama vidukari, wadudu wa kabichi na wengineo.
Tumbaku
Tumia ugoro au chemsha miche 20 ya tumbaku. Dawa hii inazuia wadudu wanaoshambulia mahindi
shambani, wadudu wanaokata miche, kupe, vidukari, viwavi na wengineo. Chukua gramu 500 za
tumbaku, changanya maji lita nane na uchemshe. Chuja baada ya kupoa, ongeza maji lita nane tena na
gramu 60 za sabuni ili kuongeza ubora.
Ni muhimu kuwa na tahadhari kwa kuwa tumbaku ni sumu kwa binadamu na wanyama, hivyo weka
mbali
na wanyama wafugwao. Inashauriwa kuvuna mazao siku 45 baada ya kunyunyiza aina hii ya dawa.