Jinsi unavyoambukiza:
- Vyakula vya kuku kutoka sehemu yenye ugonjwa kwenda kusiko na ugonjwa.
- Kuku asiye mgonjwa kula vimelea vya ugonjwa kupitia kinyesi cha kuku mgonjwa kwenye chakula.
- Mizoga ya kuku yenye ugonjwa ikipelekwa sehem isiyo na ugonjwa.
- Kuku mgonjwa huweza kurithisha vifaranga wake kupitia mayai yaliyotagwa.
- Watu na vyombo vya usafiri wanaweza kuhamisha ugonjwa kutoka sehem hadi sehemu.
Dalili za ugonjwa huu ni;
- Homa Kali
- Kinyesi kuonekana kuganda sehem za nyuma.
- Kiwango cha utagaji hushuka.
- Manyoya husimama
- Kuku kudhoofika
- Kukosa hamu ya kula.
Kinga:
Tenganisha vifaranga na kuku wakubwa.Kuku wagonjwa watengwe na kupewa tiba ya antibiotic.Zingatia usafi wa banda na vyombo vya chakula na maji.
Tenganisha vifaranga na kuku wakubwa.Kuku wagonjwa watengwe na kupewa tiba ya antibiotic.Zingatia usafi wa banda na vyombo vya chakula na maji.