FAHAMU KUHUSU MAGONJWA YA KUKU NA NAMNA YA KITIBU MAGONJWA YAO

Share:
Kuku hushambuliwa na magonjwa mbalimbali ambayo mengine yanatibika kwa dawa na mengine hayana tiba. Kuku hushambuliwa na magonjwa mbalimbali ambayo mengine yanatibika kwa dawa na mengine hayana tiba.

Magonjwa ya kuku na tiba zake ni kama zifuatazo;

NDUI YA KUKU (Fowl Pox)

Ugonjwa huu husababishwa na virusi.

Dalili za ugonjwa huu ni;
    -Kuku hupatwa na vidonda kichwani.

    -Kuku hupata uvimbe mweupe kwenye mdomo na kushindwa kula.

Tiba za ugonjwa ndui
 Ugonjwa huu hauna tiba.
Kinga za ugonjwa huu.

Chanja kuku wako wa siku 60-90 kwa chanjo ya Ndui ya kuku (Fowl pox vaccine).i.

GUMBORO
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.

Dalili za ugonjwa
    -Kuku kuzubaa na kulundikana, pamoja na kusinzia
    -Kuku kuharisha

    -Kuwa na vifo vingi kwa kuku

Tiba.

Ugonjwa huu hauna tiba,,Kuku wakipewa Dawa za oxytetracycline hupunguza vifo.

Kinga  

wakinge kuku wapo kwa kuwapa chanjo ya gumboro (Gumboro vaccine)

MDONDO

   Ugonjwa huu husababishwa na virusi

Dalili za ugonjwa wa mdodndo
  -Ugonjwa huu hutokea kwa ghafla na kuenea kwa haraka
  -Vifo vya kuku huwa vingi
  -kuku hupumua kwa  shida
  -Kuku hupooza na kulemaa miguu
  -Kuku hupinda shingo yake
  -Kuku hupunguza kutaga mayai
  -kuku huarisha

  -Kuku Kuzunguka zunguka na kutembea kinyume nyume.

Tiba za ugonjwa za mdondo

Hauna tiba

Kinga za ugonjwa wa mdondo.

Chanja vifaranga wako na kuku wako kwa chanjo ya Mdondo (New castle vaccine) na urudie chanjo hii kila baada ya miezi mitatu.

MAHEPE (Marecks)

Ugonjwa huu husababishwa na virusi

Dalili za ugonjwa.

-Kuku hupata ulemavu na vifo vya mara kwa mara.
   
Tiba za ugonjwa huu.

 Ugonjwa huu hauna tiba

Kinga za ugonjwa huu.

Chanjo hutolewa kwa vifaranga wenye umri wa siku moja,vifaranga hupewa chanjo ya mahepe (Marecks vaccine)