Kufuga
nyuki na kuzalisha asali kwa mtindo wa kisasa kwa kujenga nyumba ya
nyuki inamwezesha mfugaji kuongeza uzalishaji pamoja na kipato.
Nyumba
ya nyuki
Hii ni aina mpya ya ufugaji wa nyuki ambapo unaweza kujenga kibanda au nyumba kisha kuweka mizinga idadi unayohitaji.
Hii ni aina mpya ya ufugaji wa nyuki ambapo unaweza kujenga kibanda au nyumba kisha kuweka mizinga idadi unayohitaji.
Ni
kwa nini kujenga nyumba au kibanda?
Ni
muhimu kufuga nyuki kwenye kibanda au kwenye nyumba kwa sababu
inasaidia kudhibiti wizi wa mizinga, pamoja na wanyama wanaokula
asali na kudhuru nyuki.
Inarahisisha
utunzaji wa mizinga na kuwafanya nyuki wasihame kwenda sehemu
nyingine.
Inasaidia
watu wengi kujifunza namna nzuri ya ufugaji wa nyuki, ikiwa ni pamoja
na watoto, jambo ambalo linafanya shughuli hii kuwa endelevu.
Ufugaji
wa aina hii unasaidia kuwak inga nyuki dhidi ya majanga kama vile
moto, na mafuriko.
Inawaepusha
nyuki na usumbufu unaoweza kuwafanya wasizalishe kwa kiwango
kinachotakiwa.
Uzalishaji
unaongezeka. Hii ni kwa sababu mizinga inayotumika ni ile ya
kibiashara. Mzinga 1 unapata asali kilo 30 sawa na lita 20.
Chumba
cha nyuki Aina ya nyumba
Unaweza kujenga nyumba yenye upana wa futi 3 na urefu wa futi 9. Nyumba hii inaweza kuchukua mizinga hamsini. Halikadhalika, unaweza kujenga kibanda chenye ukubwa sawa na huo.
Unaweza kujenga nyumba yenye upana wa futi 3 na urefu wa futi 9. Nyumba hii inaweza kuchukua mizinga hamsini. Halikadhalika, unaweza kujenga kibanda chenye ukubwa sawa na huo.
Eneo
linalofaa
Ili
kuwa na ufanisi mzuri, nyumba hii inafaa kujengwa nje kidogo ya
makazi ya watu.
Kusiwe
na mifugo karibu.
Iwe
sehemu ambayo watoto hawawezi kufika.
Isiwe
karibu na njia ambayo watu wanapita mara kwa mara.
Kusiwe
na aina ya mimea ambayo nyuki hawapendi.
Kuwe
na maji karibu.
Mavuno
Baada
ya kujenga nyumba, kuweka mizinga na nyuki kuingia, unaweza kuvuna
kwa mara ya kwanza baada ya miezi mitatu. Utaweza kupata mavuno
mazuri endapo utavuna kabla nyuki na wadudu wengine hawajaanza kula
asali.
Ni
muhimu kuhakikisha kuwa wadudu waharibifu kama vile sisimizi, mende
na wengineo wanadhibitiwa ili kutokuathiri uzalishaji wa asali.
Hakikisha unavuna kitaalamu ili kuepuka upotevu wa asali. Endapo
nyuki wametunzwa vizuri na kwenye mazingira mazuri, unaweza kuvuna
asali mara tatu kwa mwaka. Katika mzinga mpya nyuki wana uwezo wa
kutengeneza masega kwa siku tatu na kuanza uzalishaji wa asali.